Pages

Sunday, July 15, 2012

Dkt. Selemani Sewangi ateuliwa Katibu Mkuu Mtendani wa BAKITA

Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dkt. Fenella Mukangara amemteua Dkt. Selemani Sewangi (55) kuwa Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili la Taifa (BAKITA).

Kwa mujibu wa taarifa ya Waziri, uteuzi huo umeaanza rasmi Julai Mosi mwaka huu.

Dkt. Sewangi ni Mhadhiri Mwandamizi wa Taasisi za Kiswahili kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Dkt. Sewangi anachukua nafasi iliyoachwa na Dkt. Anna Kishe aliyestaafu kwa mujibu wa sheria.

Popular Posts