Pages

Sunday, July 15, 2012

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma za Jamii Yatembelea NHIF

Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii,Mh. Dk. Hussein Mwinyi akizungumza na wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma za Jamii iliyofanya ziara yale leo kwenye makao makuu ya Mfuko huo yenye lengo la kujifunza mambo mbali mbali yanayofanya na Mfuko huo.
Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma za Jamii,Mh. Dk. Faustine Ndungulile akizungumza na wajumbe wa kamati hiyo na viongozi wakuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) wakati kamati yake ilipofanya ziara katika makao makuu ya Shirika hilo yaliyopo Kurasini,jijini Dar es Salaam.
Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma za Jamii na Mbunge wa Jimbo la Korogwe Vijijini,Mh. Steven Ngonyani "Prof. Maji Marefu akisalimia wadau.
Mjumbe wa Kamati hiyo na Mbunge wa Jimbo la Nzega, Dk. Hamisi Kigwangalla nae akisalimia wadau.
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF),Ndg. Emmanuel Humba akitoa maelezo mafupi kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma za Jamii.
Mwenyekiti wa Bodi ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF),Mh. Deogratius Mtukamazina (kulia) akitoa salamu ya Bodi yake kwa Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma za Jamii iliyofanya ziara yale jana kwenye makao makuu ya Mfuko huo yenye lengo la kujifunza mambo mbali mbali yanayofanya na Mfuko huo.Wengine pichani ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati Kudumu ya Bunge ya Huduma za Jamii,Mh. Dk. Faustine Ndungulile,Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii,Mh. Dk. Hussein Mwinyi,Naibu Waziri wa Afya, Dk. Sirra Umbwa,Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI),Mh. Majaliwa K. Majaliwa.
Baadhi ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma za Jamii wakifuatia kwa makini maelezo yaliyokuwa yakitolewa ukumbini hapo.
Meneja wa Idara ya Uanachama wa NHIF,Bi. Ellentruder Mbogoro akielekeza jambo kwa Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma za Jamii walipotembelea makao makuu ya Mfuko huo,Kurasini jijini Dar es Salaam jana.
Afisa Nyaraka wa NHIF,Erastus Msigwa akiwaonyesha Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma za Jamii moja ya mafaili ya Wanachama wa Mfuko huo yaliyohifadhiwa kwenye Masanduku ya Kisasa yanayotumia mfumo wa Umeme.

Popular Posts