Pages

Monday, July 16, 2012

MKUTANO WA VIONGOZI WA CCM MKOANI KATAVI

Naibu Waziri TAMISEMI,Mh.Aggrey Mwanri akihutubia wananchi wa Mpanda mkoani Katavi,ambapo aliwasihi kutokubali kudanganywa danganywa na pia aliwaambia wananchi serikali hii isingependa kuona wananchi wa chini akionewa, hivyo alitoa tamko la kutowalipisha ushuru wakina mama wafanya biashara ndogo ndogo mfano vitumbua na chapati.
Naibu Waziri Kilimo na chakula,Mh. Adam Malima akihutubia wananchi wa mkoa wa Katavi, juu ya masuala mabali mbali ambayo yametekelezeka likiwemo suala la umeme na pia aliwaambia wakulima kwamba serikali imeandaa utaratibu mzuri wa vocha za kilimo ambazo utatangazwa hivi karibuni.
Naibu Waziri Wizara ya Uchukuzi,Mh. Charles Tizeba akizungumzia masuala ya kuimarisha reli na pia utunzaji wa treni zetu ikiwa suala zima la usafi, pia aliwaambia wananchi serikali imeagiza mabehewa ya abiria na ya mizigo.
Mh.Nape akihutubia wananchi wa Mpanda waliofurika kwenye uwanja wa Kashaulili,ambapo alikemea vikali vitendo vya vyama vingine kuendekeza vurugu badala ya siasa.
Mh.Mwigulu Mchemba akieleza wananchi masuala muhimu ya kiuchumi na kwa nini kunakuwa na mfumuko wa bei,pia alitumia fursa hiyo kukemea mauaji yalotokea kwenye jimbo lake ambapo kijana mmoja kiongozi wa chama aliuawa na wanachama wa chama cha upinzani
Viongozi wakuu wa Chama cha Mapinduzi wakishiriki maandamano kuelekea kwenye uwanja wa Kashaulili wilaya ya Mpanda.
Katibu wa Halmashauri Kuu Taifa-Itikadi na Uenezi, Mh. Nape Nnauye akisalimiana na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi wa wilaya ya Mpanda, mkoa wa Katavi

Popular Posts