Pages

Saturday, July 28, 2012

SAFINA RADIO YA ARUSHA YAOMBEA TAIFA

Kituo cha Redio cha Safina cha jijini Arusha leo kimeandaa kusanyiko kubwa la neon la Mungu ambalo limelenga kuomboleza Taifa la Tanzania na kuongozwa na kichwa kisemacho TOBA YA TAIFA “Tubuni Dhambi zenu zifutwe” Maneno kutoka Matendo 3:19.

Kivutio kikubwa katika mkutano huu ni pale wananchi waliokuwa wakifika hapo wakiwa wamevaa magunia na viroba nah ii ni kutokana hasa na neon lenyewe lilivyokuwa likiwataka kufanya hivyo. Ambalo ni “Kwa sababu hiyo jifungeni nguo za magunia; ombolezeni na kulia kwa uchungu; kwa maana hasira kali ya Bwana haikugeuka na kutuacha”.
Mtumishi wa Mungu, Jovin Abel Msuya kutoka Safina Radio, akitoa neon la Mungu kwa wakazi wa Arusha na Vitongoji vyake waliofurika katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid mjini hapa leo kuomboleza juu ya taifa la Tanzania.
Umati wa wakazi wa Arusha na vitongoji vyake wakiwa uwanjani hapo wakipokea neno la Mungu.
Bibi huyu nae alijitokeza uwanjani hapo na Biblia yake akifuatilia neno na kuomboleza juu ya taifa lake la Tanzania.
Yalikuwa ni mafundisho muhimu sana na walio na madaftari walinukuu maandiko yaliyo kuwa yakitolewa kwa tafakuri zaidi.
Watoto nao hawakuachwa nyumbani katika maombolezo haya nao walikuwepo uwanjani hapa na wazazi wao.
Watu wakivaa viroba tayari kwa kushiriki mkutano wa maombolezo. Kiroba kimoja kilikuwa kinauzwa Tsh 1,000/= na vijana wengi waliviuza sana.
Wanahabari kutoka Star TV na ITV wa mjini Arusha wakiwa uwanjani hapo kutafuta habari za hapa na pale
Akina mama ndio mara nyingi hushiriki kikamilifu katika maombolezo juu ya tukio lolote na leo akina mama walikuwa wengi sana kuliko akina baba.
wanafunzi nao walishiriki mkutano huu wa Maombolezo juu ya Taifa la Tanzania
Mtumishi wa Mungu, Jovin Abel Msuya akiendelea kushusha maandiko juukwaani
Jua lilikuwa lina waka na wanafunzi baade walila.

Popular Posts