Pages

Saturday, July 21, 2012

WARAKA KWA MADIWANI WA CCM NA TLP KUHUSU MGOGORO WA MEYA ARUSHA MJINI

WAHESHIMIWA MADIWANI,
CCM NA TLP
HALMASHAURI YA MANISPAA YA ARUSHA

YAH: MGOGORO WA MEYA ARUSHA MJINI

Tafadhali husika na kichwa cha habari hapo juu.
Sisi Madiwani wa CHADEMA tumefikiri na kutafakari kwa kina kuhusu mustakabali wa maendeleo ya wananchi wa Manispaa ya Arusha Mjini. Kwa nafasi yetu ya wawakilishi na utetezi wa wananchi Arusha kwa umoja wetu ni vema tufikiri na tutafakari kwa kina kwa pamoja hasa kipaumebele ikiwa ni kutanguliza HAKI na MAENDELEO katika kumlenga kila mkazi wa aliyepo katika Halmashauri yetu. NI vema tukawa WAKWELI na WAZELENDO kwa wananchi wetu wa Arusha, huku wote tukijua kwa kina kile kilichotokea Arusha.

Kwa muda mrefu kumekuwa na mgogoro wa Uchaguzi wa MEYA wa manispaa ya Arusha, ambayo ilitokana na ukiukwaji wa kanuni na taratibu za uchaguzi wa Meya ambayo akidi yake ilikuwa haijatimia. Ikumbukwe kuwa Mhe. Kivuyo ambaye katika sakata hilo alijikuta akichaguliwa kwa hila kuwa NAIBU MEYA, alifikia hatua ya kujizulu nafasi hiyi na kukiri mbele ya waandishi wa habari na wananchi wa Arusha kuwa uchaguzi uliofanyika haukuwa wa haki na yeye alipewa nafasi hiyo kwa hila, kitu ambacho baada ya tafakari ya kina aliamua kujiuzulu ili asiwe sehemu ya dhambi hiyo na kujikuta anakalia KITI CHA DAMU. Jambo hili pia limekuwa likisemwa na baadhi ya madiwani wa CHAMA CHA MAPINDUZI pindi tunapokutana nao kuwa mfumo wa chama cha CCM unazuia kuyatamka haya lakini ukweli ni kuwa huo uchaguzi wa meya uliofanyika na Mhe Gaudence Lyimo kupata nafasi hiyo ulikuwa batili kwa mujibu wa kanuni, lakini mbaya zaidi, umepelekea damu kumwagika, jambo ambalo ndio baya.

Wote tunashuhudia jinsi ambavyo mgogoro huu ulivyo na madhara makubwa sana kwa wananchi wetu na sisi pia ambao ni sehemu ya jamii hiyo hiyo. Mbali na kusababisha watu watatu kupoteza maisha, pameendelea kutokea sintofahamu kubwa kutoka kwa wananchi jambo ambalo limeendelea kuzidisha hasira kwa wananchi kwa serikali. Jambo hili ni vema likafanyiwa kipimo maana mchezo huu na hila hii inaweza kuzaa balaa ambalo sio rahisi kulimudu tena.

Dharau na makusudi yanayofanywa na chama cha mapinduzi, mathalani Mhe Gaudence Lyimo na MKURUGENZI wa halmashauri katika kupuuzia wito wa CHADEMA kuwa HAKI haikutendeka, KANUNI zilivunjwa na hivyo uchaguzi wa MEYA ufanyike upya kwa kufuata kanuni sasa inafika mahali haivumiliki na hapo ndipo itakuwa mikononi mwa wananchi na sio CHADEMA tena.

Sambamba na hali hii, pia mgogoro huu unatumiwa na watendaji wa Halmashauri kufanya mambo yao yasiyo ya kiuadilifu kwani hakuna udhibiti wa kabisa katika uendeshaji wa halmashauri yetu. Waheshimiwa madiwani, katika ukweli huu, MKURUGENZI na huyo anayeitwa MEYA watatoa wapi ujasiri na kujiamini “moral authority” ili hali wao wameshiriki dhambi mbaya ya kuchakachua kanuni za kufanya uchaguzi wa meya isivyo halali na mbaya zaidi Mhe Gaudence kuendelea kung’ang’ania nafasi hiyo kwa kiwango cha damu ya watu kumwagika bila hata kujali??

Hata hivyo, hata kama Mhe Gaudence Lyimo hatajali wito huu ambao kwetu ni wito wa mwisho kwake na chama chake, jambo hili tunaliacha kwa MUNGU mwenye HAKI atashughulika nae kwa wakati wake na muda si mrefu tutapata majibu ya maombi yetu. Pili tunaliacha jambo hili kwa wananchi ili waamue kwa sababu wameshajua wazi kuwa Mhe Gaudence Lyimo na chama chake waliamua na wameendelea kuwafanyia uhuni katika mji wao. Sisi tumeliacha kwao waamue watakavyoamua.

Tunafahamu kabisa katika nafsi na mioyo yenu mnafahamu uchaguzi haukuwa halali lakini mnashindwa kusimamia ukweli kwa sababu ya ubinafsi na kukosa uzalendo kwa wananchi wa Arusha kwa kutanguliza maslahi yenu mbele, kitu ambacho tusingependa kipewe tafsiri hiyo
Tunawasihi kwa dhati kabisa tuamue kwa pamoja kwa manufaa ya Arusha tukubaliane kama viongozi wazalendo, wapenda maendeleo na wenye hofu ya MUNGU tufanye uchaguzi wa MEYA wa Halmashauri ya Arusha ambao utakuwa ni halali kwa vyama vyote.

Nchi nyingi za Afrika kumekuwa na vita vya wao kwa kwao kwa sababu ya uchu wa madaraka. Hili limetokea pia hapa Arusha watu wamekufa kwa sababu ya MEYA, hii ni aibu na ni dhambi kwa kung’ang’ania madaraka ambayo si haki.

Waheshimiwa madiwani wenzetu hata juhudi za serikali kufanya maendeleo wananchi wengi wa Arusha bado hawana imani na serikali yao kwa sababu ya MEYA tu. Hivi sasa kuna mradi wa ujenzi w barabara unaondelea ukweli ni kwamba jambo hili ni zuri lakini wananchi wanalibeza sana kama vile linafanywa kwa hila. Kwa nini iwe hivi??

Kimsingi tunataka MEYA ambaye yupo huru kutembelea kata zote kwa ajili ya maendeleo bila kujali itikadi ya chama chake. Hatutaki MEYA anayevizia misiba na harambee.
Mwisho tunamwomba Mh. Gaudence Lymo atafakari kwa kina kwa kumuomba MUNGU wake ampe hekima na ujasiri wa kuchukua maamuzi magumu ya kujiuzulu nafasi ya UMEYA na uchaguzi wa kidemokrasia ufanyike kwani utampa heshima na amani katika maisha yake yote.
Tunaomba Waheshimiwa Madiwani wenzetu kwa pamoja tuseme dhambi hii imetosha na tutubu kwa kufanya uchaguzi wa haki na Amani. Na kwa dhati kabisa yeyote atakayechaguliwa hata kama ni Mh. Gaudence tutampa ushirikiano wa dhati kabisa.

Tunaomba ushirikiano wenu katika jambo hili ambalo ni la msingi kwa maendeleo ya watu Arusha. Kila mmoja kwa imani yake aombee jambo hili kwani halitaki ushabiki linahitaji utulivu wa akili.

WAHESHIMIWA MADIWANI, FANYENI TAFAKARI YA KINA, ZINGATIENI JINSI WANANCHI KATIKA KATA ZENU WANAVYOWATAZAMA, ni matumaini yetu kuwa tutafanya uchaguzi wa MEYA ndipo tufanye uchaguzi wa Naibu MEYA. Na jambo hili litakuwa ni ushindi na sifa iliyotukuka kwa MADIWANI WOTE na sio kundi fulani la watu.

Asanteni sana

Doita Isaya Harri
Mwenyekiti madiwani wa CHADEMA

Nakala:
Katibu wa CHADEMA (M)
Katibu wa CCM (M)
Katibu wa TLP (M)
Mkurugenzi wa Halmashauri – Arusha Mjini

MAELEZO KUHUSU FAO LA KUJITOA KATIKA MAREKEBISHO YA SHERIA ZA MIFUKO YA HIFADHI YA JAMII

Makamu wa Rais, Corporate Affairs
Barrick Gold
S.L.P 1081
Dar-es-Salaam

UFAFANUZI KUHUS FAO LA KUJITOA KATIKA MAREKEBISHO YA SHERIA ZA MIFUKO YA HIFADHI YA JAMII.

Ufuatao ni ufafanuzi mfupi kuhusu marekebisho ya Sheria za Mifuko hasa kuhusu fao la kujitoa.

1. Kama mtakumbuka Sheria za Mifuko ya Hifadhi ya Jamii pamoja na Sheria ya Mamlaka zimefanyiwa marekebisho na kupitishwa na Bunge tarehe 13 Aprili, 2012. Sheria hiyo tayari imeshasaininiwa na Mheshimiwa Rais na imeanza kutumika rasmi. Marekebisho haya yanawahusu wafanyakazi wote nchini mwetu bila kubagua sekta yoyote ile.

2. Kwa mujibu wa marekebisho hayo fao la kujitoa (withdrawal benefits) yamefutwa na kuanzia sasa hayatakuwepo. Mafao hayo yalikuwa yanatolewa pale mwanachama alipokuwa anaacha kazi. Sasa mwanachama wa Mfuko atapata mafao yake pale atakopfikisha umri wa kustaafu kwa hiari (miaka 55) au kwa lazima (miaka 60) au pale anapopata ulemavu wa kudumu.

3. Kwa kuzuia fao la kujitoa mwanachama anapata fursa ya kupata mikopo ya nyumba kwa kutumia dhamana ya michango yake kama ilivyoelezwa kwenye Sheria ya SSRA kipengele cha 38.

4. Marekebisho hayo kuhusu kuzuia mafao ya kujitoa yamefanyika ili kutimiza lengo na madhumuni ya hifadhi ya jamii ambayo ni kuhakikisha kuwa mwanachama anapostaafu anapata mafao bora yatakayomwezesha kumudu maisha ya uzeeni wakati ambapo nguvu ya kufanya kazi tayari imeshamwishia. Mafao ya kujitoa yanapunguza na hata kuondoa kabisa kinga ya mfanyakazi pale anapoumia kazini au anapofika uzeeni.

5. Tunawaomba muwaelimishe wafanyakazi umuhimu na madhumuni ya mafao ya hifadhi ya jamii. Hifadhi ya jamii ni nyenzo mahususi iliyowekwa kuwasaidia

1

wafanyakazi kuendesha maisha yao wakati wanapokuwa wameishastaafu tayari. Umasikini wa kipato wakati wa uzee ni mojawapo ya changamoto ngumu kukabiliana nazo kwa mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla. Tunawasihi tena muelimishe wafanyakazi kuhusu jambo hili. Tafadhali msisite kuwasiliana na Mamlaka pale ufafanuzi zaidi utakapohitajika

6. Kwa kuwa marekebisho hayo yamesainiwa na kuanza kutumika rasmi kama sheria, mafao ya kujitoa hayawezi kutolewa tena na wafanyakazi watakaoacha kazi kwa sababu ya marekebisho ya kipengele hicho watakuwa hawajaijitendea haki wao wenyewe na pia itakuwa ni kunyume cha Sheria. Mamlaka inaandaa kanuni za mafao ambayo lengo lake ni kuboresha maslahi ya wanachama, kanuni hizo zitajadiliwa na wadau wakiwemo vyama vya wafanyakazi na waajiri ili kupata maoni yao.

7. Tafadhali muwaelimishe wafanyakazi kwamba pamoja na kuzuia fao la kujitoa, mafao mengine ambayo ni muhimu kwa sekta ya Madini yataendelea kutolewa kama kawaida. Mafao hayo ni Kama vile kuumia kazini pamoja na fao la ulemavu

8. Tumesikia kwamba tayari kuna hofu imejijenga kwa wanachama kuhusiana na fao la kujitoa. Ikumbukwe kwamba baadhi ya Mifuko ilikuwa inatoa fao hilo kinyume cha Sheria kwani katika Sheria zao hakuna fao la kujitoa. Tunapenda kusisitiza kwamba wanachama wawe watulivu wakisubiri miongozo.

9. Tunapenda kuwahakikishia kwamba katika hili maslahi ya wanachama yatalindwa na hakuna mwanachama atakayepunjika kutokana na utaratibu huo. Mamlaka imepanga kutembelea wafanyakazi wa sekta ya madini katika juma la kwanza la mwezi Agosti 2012 ili kutoa ufafanuzi zaidi kwa wanachama wote.

Tunatanguliza shukrani za dhati kwa ushirikiano.


Wenu.
Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Hifadhi ya Jamii

Managing Director Of National Bank Of Commerce(NBC)Mr Lawrence Mafuru Has Been Requested and Accepted to go on Leave un Orderi to Allow Investigations

Managing Director Of NBC, Lawarance Mafuru
--
Editors Note;
NBC is one of the most represented retail bank in the country with 45 years experience in providing financial services. Apart from offering traditional banking services, NBC also prides itself with an expanded branch network and footprint. NBC has 53 branches, 287 Visa enabled ATMs, and over 233 Points of Sales strategically located throughout the country. NBC has employed over 1400 staff

For more information contact
Mwinda Kiula-Mfugale,
Head of Marketing, Communications and Corporate Affairs: Mwinda.Kiulamfugale@nbctz.com

NSSF na ZSSF Zatoa mchango wa Milioni 10 kwa wahanga wa Ajali ya Meli

Afisa Muandamizi wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii Tanzania Nd. Juma Kimtu akimkabidhi Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi Mchango wa Maafa wa Shilingi 10,000,000/- hapo ofisini kwake Mbweni nje kidogo ya mji wa Zanzibar. Nyuma yake ni Meneja Msuluhishi wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar { ZSSF } Nd. Khamis Phil Phil Than.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akipokea mchango wa Maafa wa shilingi 10,000,000/- kutoka kwa Meneja Msuluhishi wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar { ZSSF } Nd. Khamis Phil Phil Than hapo katika Ofisi yake iliyopo Baraza la Wawakilishi Mbweni nje kidogo ya Mji wa Zanzibar.
---
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi amewanasihi Wananchi kuendelea kuiamini Serikali katika kupokea Taarifa zake hasa wakati wa kutokea Majanga na Maafa.

Nasaha hizo amezito hapo katika Ofisini yake iliyopo Baraza la Wawakilishi Mbweni nje kidogo ya Mji wa Zanzibar wakati akipokewa mkono wa Pole kutoka kwa Taasisi mbali mbali za Umma na Kijamii.

Salamu hizo za mkono wa pole zimetolewa kwa Balozi Seif na Uongozi wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar { ZSSF } na ule wa Hifadhi ya Taifa ya Jamii ya Tanzania { NSSF } ambapo kila moja ilikabidhi mchango wa Shilingi Milioni kumi { 1,000,000/- }.
Balozi Seif alisema Jamii kujenga tabia ya kuiamini Serikali hupelekea kuwepuka kuchanganywa wakati wa kupokea Taarifa hizo kutoka vyombo vya Habari vinavyopokea Baadhi ya Taarifa zisizo rasmi.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar aliupongeza Uongozi wa mifuko hiyo ya Hifadhi ya Jamii Bara na Zanzibar kwa kufikiria jambo hilo muhimu la kutoa mchango ambalo Taifa linahitaji kuungwa mkono katika kukabiliana nalo.

Aliuhakikishia Uongozi wa Taasisi hizo kwamba michango hiyo itasimamiwa vyema kwa ajili ya kuwafika waliohusika kwa kutumia utaratibu uliotumika wakati wa ajali iliyotokea Mwaka jana.

Alisema licha ya zoezi la uokozi kuwa na gharama kubwa lakini Serikali inaendelea kutoa huduma zote za mazishi na usafirishaji wa maiti zinazopelekwa Tanzania Bara ambazo zilipatikana kutokana na ajali ya Meli ya M.V Skagit hapo juzi.

Aliongeza kuwa shughuli hiyo ikiwemo gharama za vyombo, mafuta, Chakula na uokozi zinahitaji kuungwa mkono na taasisi na jumuiya ya kiraia ndani na nje ya Nchi. “ Serikali imeshachukua jukumu la kuzizika zile Maiti zilizoshindwa kutambulika hadi sasa, kuzisafirisha maiti tatu hadi Tanzania Bara pamoja na familia nne wakati maiti moja ya raia wa kigeni bado haijatambulika”. Alifafanua Balozi Seif.

Alisisitiza kwamba katika juhudi za kukabiliana na tatizo hilo wazamiaji wa Israel walioko Nungwi Mkoa wa Kaskazini Unguja wameamua kusaidia kazi ya uokozi kwenya Meli hiyo ili kuendelea kutafuta miili ya Watu iliyopotea.

Mapema Meneja Msuluhishi wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar { ZSSF } Ndugu Khamis Phil Phil Than alisema yapo mambo mengi kwenye tukio hilo la Maafa ambayo yanahitajika kupata msukumo kutoka kwa Washirika, Taasisi na Jumuiya za Kiraia. Ndugu Phil Phil alisema mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar umekuwa mstari wa mbele katika kutekeleza majukumu yake yaliyolenga zaidi kwenye eneo la Jamii.

Naye kwa upande wake Ofisa Muandamizi wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii Tanzania { NSSF } kutoka Makao Makuu Mjini Dar es salaam Nd. Juma Kimtu alimueleza Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar kwamba Taasisi hiyo imeamua kutoa mchango huo baada ya kuona uzito Maafa yaliyotokea ambayo yameigusa Jamii yote.

Ndugu Kimtu alisema Serikali kwa kuwa ni ya watu haina budi wakati wote kusaidiwa hasa katika masuala ya Majanga na Maafa ambayo kwa kiasi kikubwa huigusa Jamii yote.
Na
Othman Hamisi Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili Wa Rais Zanzibar

NSSF na ZSSF Zatoa mchango wa Milioni 10 kwa wahanga wa Ajali ya Meli

Afisa Muandamizi wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii Tanzania Nd. Juma Kimtu akimkabidhi Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi Mchango wa Maafa wa Shilingi 10,000,000/- hapo ofisini kwake Mbweni nje kidogo ya mji wa Zanzibar. Nyuma yake ni Meneja Msuluhishi wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar { ZSSF } Nd. Khamis Phil Phil Than.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akipokea mchango wa Maafa wa shilingi 10,000,000/- kutoka kwa Meneja Msuluhishi wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar { ZSSF } Nd. Khamis Phil Phil Than hapo katika Ofisi yake iliyopo Baraza la Wawakilishi Mbweni nje kidogo ya Mji wa Zanzibar.
---
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi amewanasihi Wananchi kuendelea kuiamini Serikali katika kupokea Taarifa zake hasa wakati wa kutokea Majanga na Maafa.

Nasaha hizo amezito hapo katika Ofisini yake iliyopo Baraza la Wawakilishi Mbweni nje kidogo ya Mji wa Zanzibar wakati akipokewa mkono wa Pole kutoka kwa Taasisi mbali mbali za Umma na Kijamii.

Salamu hizo za mkono wa pole zimetolewa kwa Balozi Seif na Uongozi wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar { ZSSF } na ule wa Hifadhi ya Taifa ya Jamii ya Tanzania { NSSF } ambapo kila moja ilikabidhi mchango wa Shilingi Milioni kumi { 1,000,000/- }.
Balozi Seif alisema Jamii kujenga tabia ya kuiamini Serikali hupelekea kuwepuka kuchanganywa wakati wa kupokea Taarifa hizo kutoka vyombo vya Habari vinavyopokea Baadhi ya Taarifa zisizo rasmi.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar aliupongeza Uongozi wa mifuko hiyo ya Hifadhi ya Jamii Bara na Zanzibar kwa kufikiria jambo hilo muhimu la kutoa mchango ambalo Taifa linahitaji kuungwa mkono katika kukabiliana nalo.

Aliuhakikishia Uongozi wa Taasisi hizo kwamba michango hiyo itasimamiwa vyema kwa ajili ya kuwafika waliohusika kwa kutumia utaratibu uliotumika wakati wa ajali iliyotokea Mwaka jana.

Alisema licha ya zoezi la uokozi kuwa na gharama kubwa lakini Serikali inaendelea kutoa huduma zote za mazishi na usafirishaji wa maiti zinazopelekwa Tanzania Bara ambazo zilipatikana kutokana na ajali ya Meli ya M.V Skagit hapo juzi.

Aliongeza kuwa shughuli hiyo ikiwemo gharama za vyombo, mafuta, Chakula na uokozi zinahitaji kuungwa mkono na taasisi na jumuiya ya kiraia ndani na nje ya Nchi. “ Serikali imeshachukua jukumu la kuzizika zile Maiti zilizoshindwa kutambulika hadi sasa, kuzisafirisha maiti tatu hadi Tanzania Bara pamoja na familia nne wakati maiti moja ya raia wa kigeni bado haijatambulika”. Alifafanua Balozi Seif.

Alisisitiza kwamba katika juhudi za kukabiliana na tatizo hilo wazamiaji wa Israel walioko Nungwi Mkoa wa Kaskazini Unguja wameamua kusaidia kazi ya uokozi kwenya Meli hiyo ili kuendelea kutafuta miili ya Watu iliyopotea.

Mapema Meneja Msuluhishi wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar { ZSSF } Ndugu Khamis Phil Phil Than alisema yapo mambo mengi kwenye tukio hilo la Maafa ambayo yanahitajika kupata msukumo kutoka kwa Washirika, Taasisi na Jumuiya za Kiraia. Ndugu Phil Phil alisema mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar umekuwa mstari wa mbele katika kutekeleza majukumu yake yaliyolenga zaidi kwenye eneo la Jamii.

Naye kwa upande wake Ofisa Muandamizi wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii Tanzania { NSSF } kutoka Makao Makuu Mjini Dar es salaam Nd. Juma Kimtu alimueleza Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar kwamba Taasisi hiyo imeamua kutoa mchango huo baada ya kuona uzito Maafa yaliyotokea ambayo yameigusa Jamii yote.

Ndugu Kimtu alisema Serikali kwa kuwa ni ya watu haina budi wakati wote kusaidiwa hasa katika masuala ya Majanga na Maafa ambayo kwa kiasi kikubwa huigusa Jamii yote.
Na
Othman Hamisi Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili Wa Rais Zanzibar

Friday, July 20, 2012

A Guide to Helping Africa

Helping Africa has become a self-perpetuating for profit non-profit business. It has become what Teju Cole calls the white savior industrial complex. This does raise the questions, are there ways in which help can actually be useful? Where help can actually do more good than harm and offer more than miracle water?

Here below, are ten ways, and I invite you to think of your own, through which Westerners can contribute to what Nelson Mandela in the struggle against apartheid referred to as a 'profound and irreversible change'.

1. Oppose unequal trade. For every dollar given in foreign aid, two dollars are lost through unequal trade. Instead, support concrete efforts that promote equal trade such as an end to US and European farm subsidies that unfairly depress farm markets at the expense of African farmers and their families. Africa needs equal trade not foreign aid.

2. Take responsibility for your governments. Oppose policies that will do more harm than good: for example, the US African Command Center (Africom) which will lead to the militarization of US foreign policy in Africa. Or, European and American anti-terror policies that have eroded citizen rights in African countries instead of enhancing security. Instead, support NGO's and other organizations that are working at changing US/Western foreign policies toward Africa such as Africa Action and Trans Africa Forum.

3. Oppose NGO's that will do more harm than good. For example, the Bill Gates initiative, the Alliance for Green Revolution in Africa will lead to loss of bio-diversity in addition to opening up African agriculture to GMO seeds. Instead, support efforts that call for the depolitization of food and water distribution in African countries and organizations that promote democratic approaches to food such as Food First.

4. Support African grassroot organizations that are opposed to national policies that hurt the poor e.g. Abahlali baseMjondolo, the Shackdwellers movement in South Africa. These organizations grow organically from the communities they serve and identify and cope with the problems in ways that the celebrity endorsed NGO cannnot.

5. Call for technological (scientific, internet, medical etc) democracy within and among nations.

6. Internationalize curriculum from early to university education in Western countries. This means that from an early age to adulthood, the Westerner will have an international consciousness and therefore be able to make decisions, whether it is in voting for elected officials or on which policies to support, that are informed.

7. Read what Africans read. Educate yourself on the history of the issues Africa is facing today. For example, to understand unequal trade today, read the historical book, 'How Europe Underdeveloped Africa', by Walter Rodney. To understand the complexity of women's oppression, read essays by African women such as 'Feminism with a small "f"' by Buchi Emechata , or novels such as, 'Woman at Point Zero' by Nawal El Saadawi and 'Maps' by Nurrudin Farah.

8. To access African voices on current political events, read African Independent media such as Pambazuka News and Africa Focus and consider making a financial donation. African independent media is in dire need of funding.

9. Support democracies with content. Call for African governments to complement the vote with economic, political and cultural equality.

10. Empathy in place of pity. Pity is outward and requires nothing beyond the occasional donation to an NGO. Empathy on the other hand leads to solidarity, to the realization that our fates are intertwined. If your need for security causes someone else's insecurity, and your being fed leads to someone else's hunger, the solution is not to be found in pity but in empathetic action - action that brings about irreversible people centered changes in the West and in Africa as well.

Mukoma wa Ngugi is an Assistant Professor of English at Cornell University and the author of Nairobi Heat (Melville, 2011). Please visit www.mukomawangugi.com for more information.

An Open Letter to Obama

OPINION

Here you are, brother: Caught in the wheels of history, part of processes that transform the world and part of systems that destroy it.'

Dear President Barack Obama,

I hope you don't mind me addressing you directly. I would like to call you brother, as I am known to do. Many would have me not - friends because they feel that you have left and enemies because they fear that you have not. I will, no matter, because we are of each other.

Maybe I should start with telling you who I am and why I want to address you. I am a child of a battered generation. The child of a generation whose wars were fought gallantly, with courage, at huge cost, by young people who were sent to the gallows, executed, punished for their daring. And I am of a generation who were chained to the bed from birth in punishment for the rebellion of our parents. Who were fed drugs and capitalism in equal dose of malicious silencing. You know this generation because you too are of the lost souls raised amongst the scattered bones of revolutions past and the drawn skulls of promises unfulfilled. The liberation movements of the 1960s were fading and erased by the time we saw the light but for the pained eyes of martyrs and survivors.

We were raised in the hollowed halls of neo-colonial regimes where Mobutu and Moi were called leaders in mocking irony at the memories of Machel, Cabral and Nyerere. Where Sankara and Bishop made last ditch attempts to uphold truth faced with savage reprisals by the tyranny of Thatcher and Reagan. Where Cuba was the last bastion of alternative but even the image of Ernesto fell to the commodified greed of hungry empire finding new and twisted ways to pacify revolt.

I am Black ... is no longer said with pride and resistance. But, "I am Black" is how I understand myself. I am Woman, I am Queer, I am African. Yet rainbow nations disguising patriarchal capitalism will tell me that these truths are divisive. Many would rather I hide, silence, gloss all, if not parts, of me; but it is these truths of mine that create for me an anchor - a past and a present, a home and adversaries. I am addressing you today from this standpoint, as a sister, as a fighter, as a woman who seeks to stand always on the side of justice.

When you were making your great strides in the machinery that is the U.S.A, I watched from your father's land in Kenya. I watched initially with great fear as those around me cheered in jubilation. I thought myself a coward for being so scared. I feared that, like many before you, you would become a conveniently vilified symbol of what your image does not represent. I feared for the dignity of millions of our African sisters and brothers in the U.S.A for whom promised democracy, redress and reparation have still to be realized. And I feared for your life. We heard, below your King overtones, your Malcolm words and subtle gestures, so that even veteran Black nationalists were singing your praises. And I feared their unwavering optimism, while realizing in your unmatched mobilization how ineffective we had been.

It was a hard truth to swallow. But those times taught me so much about who I am, where I am and what I am holding onto. I learnt that an anchor should hold you but cannot lead you. I learnt that Malcolm's relevance is not in our outdated Black Power salute, nor our rhetoric, not even in our unapologetic counter to a five hundred year-old system of oppression, but that his relevance is in our ability to make his words our own, today, in this time, in our own deeds.

As you ran up against the U.S political elite, the white liberal mask was lifted once again for all to see. Those of us beautiful enough to be Black Woman, neither first nor second, were not surprised by her aristocratic tantrum calling for our allegiance and the arrogance that sought to blind class and race with femininity.

I didn't believe it: 'they are not ready for a Black president' I said in bewilderment every time you crossed another milestone. I know them, I know us, and in my script of us and them, they are not ready. My script was wrong. You won. And we played Brenda's "Black President" because it was a time to join our people in celebration. And the parallels with Mandela were indeed stark. While you were never a freedom fighter, tortured nor jailed for dissent, Madiba and Barack seem to be the conciliatory faces of false, forced nations torn at the root by white supremacy.

And with my trepidation, I couldn't help but smile at the moment you offered, the smiles I saw on weary fighters, including my own mother who to this day has a portrait of you at her entrance that reads in bold letters - MR. PRESIDENT. You offered the hope you said you would, to the defeated generation and to the generation of our time. Those of us in between looked around incredulous, reminded that despite carrying the heavy load of burnt churches and promises, we could allow ourselves hope; that skepticism and vigilance, though it saved us from terror and assault, could not lift us into the light. We had been brave, those of us who soldiered on, alone carrying a fading torch of liberation in the wreckage of Aids, structural adjustment, the war on drugs and evangelism. Knowing that our people deserved fulfillment not just hope; forgetting how to ignite imagination.

I dared at that point to watch. Not for what you could make happen in the burning house, but, for what you might be able to offer the world from an increasingly belligerent empire. The world was restless, balancing at the tipping point of destruction. A simple "Assalam Alaikum" reverberated across the seas. And despite the open gestures, you were not able to stand firm in the stance of open palm, proving again that the system is stronger than the people who make it up. You stepped up the aggression in your speech, the threats in your voice and set the boat sailing again for leading through violence. The lid finally shut closed when you stood before the world to deny the Palestinian people their self-determination. So when we mourned the murder of Troy Davis that week, we also mourned every victim and survivor of U.S imperialism from Palestine to Oakland, DRC to Iraq.

And here you are, brother, caught in the wheels of history, part of processes that transform the world and part of systems that destroy it. I wonder in this hunt who will be writing history - the hunter or the lion? Whether we make gains or suffer setbacks, you have been part of the historical impetus towards the long awaited white strike against capitalism - Occupy Wall Street. Showing dissent to a system that works against most (though it is this same dissent that also created fascist leaning factions like the Tea Party), it seems the white population of the U.S is catching up to the global resistance and, in their focus on Wall Street, have avoided displaying your image as that of oppressor - acknowledging that the capitalists who fuel the engine of empire outrun presidents. But, I have seen them indeed occupy, the organizing space and tactics of poor, Black and brown revolution and already the whispers calling for decolonization of occupy.

They say that you are the first Gay president. Perhaps in an attempt to maintain Clinton's title as the first Black one - as if playing the saxophone despite enlarging the prison industrial complex, attacking working Black mothers, despite Somalia and Rwanda, makes you Black. Brother, I can't say that the gains of 'equality' that assist in integrating gay and lesbian middle-class white people into the patriarchal institution of marriage or the army feels to me like freedom.

I am certain that they are winning and that you are valiantly attempting to struggle against homophobia. But at my very core, I don't want to fit their box, no matter how glossy and new it may look or how much they tell me that parts of me are acceptable (never the whole). What my Queer politic seeks is for us all to liberate ourselves from all notions that imprison our imagination to the normativity of oppression. For us all to experience whole, free, respectful, positive and loving lives in all its dimensions, accepting plurality, complexity, and self-determination from body to nation.

So when you give the orders (or is it succumb to the orders?) to bomb Africa's North in Libya, I know that you are not the first queer president. I cried at the images of lives lost, whole cities and the continent's infrastructure destroyed. Knowing that the empires that struck with intended disdain would soon be offering debt crippling aid to 'help rebuild' what they destroyed. And now is when I hope, hope that the Libyan people will not fall to the same divide along ethnic lines that has unraveled the continent thread by thread. But, my hope was soon squashed as factions and splinters unveiled in the all too common African story as a tear falls again for the vision of our powerful unity.

African peoples are facing a full frontal assault both within and outside of empire. The financial crisis that has caused white people in the U.S widespread panic and revolt, is the same economic condition that the majority of Black people there live in during economic prosperity. One Black woman, man and child is killed every forty hours under your presidency. Our potential for revolt has been met with armed occupying forces surrounding communities in the name of policing, in the same way that home-guards patrolled villages during the Mau Mau uprising. And every time another Oscar Grant is killed, Sean Bell's murderers are acquitted, Trayvon Martin's parents cry out for justice, another Black woman jailed, we remember that Herman Bell, Leonard Peltier and Sundiata Acoli are still in jail.

On the continent, whole lands are being stolen in the name of investment, with a shockingly ahistorical adage appended to the "For Sale" sign that reads terrus nullus. Our diversity is being patented and the unsustainable pimped to us as 'the future'. The Europeans sell us 'partnership' agreements unashamedly willing a free market to exploit our resources and pimp their goods. Long gone is even mention of reparations, the paternalistic aid machinery cripples us in odious debt. While China offer 'win-win' alternatives, which no so-called leader of ours negotiates beyond the short-sighted proximity of their own pockets to translate into a win for our people and future. Meanwhile, we, the people, are so busy oppressing each other in the guise of morality, we have hardly noticed whose interests we kneel to.

Which is why there are generations like ours, a generation whose manifest destiny is seemingly and simply to remember: to carry from our grandmothers to our daughters the resistance cry of generations. Now, brother Barack, the winds of change are slowly raising the dust. And we have seen people on a move, attempting to rock the foundation of injustice. You have been a character in this determining act in the theatre of humankind. And as the curtain is drawn on African awakening spreading from Guinea, Madagascar and Mozambique to Africa's North, the world has begun to pay attention. Now is when we will all decide which way history will fall and whether the lion or the hunter will live to tell the tale. I know where you have stood, I know where I will stand.

Peace, Hakima

* Hakima Abbas is executive director of Fahamu. This article was first published by The Feminist Wire.

RISALA YA RAMADHANI YA RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI, MHESHIMIWA DK. ALI MOHAMED SHEIN

RISALA YA RAMADHANI YA RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI, MHESHIMIWA DK. ALI MOHAMED SHEIN, KWA MWAKA 1433 HIJRIYA, 2012 MILADIA.


Ndugu Wananchi,

Assalam Aleykum Warahmatullah Wabarakatuh

Alhamdu Lillahi Rabil Alamin. Shukurani zote anastahiki Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wa Viumbe vyote. Sala na Salam zimshukie Aliyetukuzwa na Muumba wetu, Mtukufu wa Daraja aliyeletwa kwa Rehema kwa ajili ya kuwaongoza waja wapate nusra ya Allah (Subhana Wataala).

Ramadhani tukufu imetufikia. Tuna wajibu wa kumshukuru Mwenyezi Mungu Azawajalla, kwa kutujaaliya umri tukaupokea Mwezi huu Mtukufu, Mwezi wa Ibada, Mwezi wa Furaha, Mwezi wa Neema. Kubwa zaidi ni kuwa huu ni Mwezi ambao kwa hekima zake Mola wetu ametuteremshia Quran, ambayo ndio “Uongofu kwa Watu” na yenye “hoja zilizo wazi za uwongofu na upambanuzi”. Aidha, ametutengezea usiku wa cheo kitukufu” usiku huo wa “Laylatul Qadri ni bora kuliko miezi elfu”.

Ndugu Wananchi,
Kutokana na neema hizi, sote tunawajibika Kwake kwa vitendo. Hivyo basi, madhumuni ya risala hii ni kuukaribisha Mwezi huu Mtukufu wa Ramadhani na kukumbushana baadhi ya mambo tunayostahiki kuyafanya katika Mwezi huu Mtukufu ili tufanikiwe hapa duniani na akhera twendako.

Wakati tunaukaribisha Mwezi Mtukufu wa Ramadhan, Mwenyezi Mungu ametupa mtihani wa maafa kwa kuzama meli ya MV SKAGIT iliyokuwa inasafiri kutoka Dar es Salaam kuja Zanzibar. Hadi jana usiku Watu wapatao 31 wamefariki, 123 hawajaonekana baada ya meli hiyo kuzama na kwa uwezo wa Mwenyezi Mungu watu 136 wameokolewa. Kuanzia asubuhi ya leo hadi mchana huu jumla ya maiti 22 zimepatikana. Katika kipindi hiki tumuombe Mola wetu atupe rehema zake, atughufirie makosa yetu na atujaalie subira.

Ndugu Wananchi,
Mwenyezi Mungu ametupa maelekezo kamili ya Mwezi huu Mtukufu katika Quran tukufu, surat Al-Baqara aya 183 hadi 187, aya ambazo Mashekhe na Maimamu wetu wamekuwa wakizielezea tangu Mwezi wa Shaaban na wanaendelea kutufundisha katika kipindi hichi na kutoa mawaidha yao.

Ndugu Wananchi,
Mafanikio ya wanadamu duniani yanakuwa makubwa kutokana na kuwa na mipango mizuri na madhubuti. Serikali zote duniani zinaendeshwa katika mtindo huo wa kujipanga na sisi hapa Zanzibar tunafanya hivyo hivyo. Mipango mbali mbali kama vile Mpango wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umasikini (MKUZA), Dira 2020 na mengineyo ni miongoni mwa utaratibu huo. Lakini mipango tu haiwezi kutuletea mafanikio bila ya kuwepo mikakati ya utekelezaji, usimamizi mzuri na juhudi za utekelezaji. Wahenga walisema Mipango si matumizi”.

Jitihada mbali mbali zimekuwa zikifanywa na Serikali katika kuimarisha ustawi wa wananchi mmoja mmoja, vikundi na wananchi wote kwa jumla tukiwa na lengo kuu la kuwapunguzia wananchi wetu ukali wa maisha. Kwa mfano, Serikali imeamua kuwapunguzia gharama za Kilimo wakulima wetu na kuimarisha huduma hiyo ili kuwasaidia wananchi kuongeza kipato chao na kupunguza utegemezi wa chakula kutoka nje ya nchi. Kadhalika, hatua hii imelenga kupunguza tatizo la mfumko wa bei hasa kwa bidhaa za chakula.

Aidha, napenda kuwashukuru wakulima wetu kwa kujiandaa kuwapa huduma nzuri wananchi wetu hasa katika upatikanaji wa chakula kwa ajili ya futari. Naamini kuwa hisani, ukarimu na kuhurumiana vitazingatiwa katika biashara na utoaji wa huduma kwenye kipindi hiki cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani. Serikali nayo itajitahidi kufanya kila linalowezekana ili kuwasaidia wananchi katika kukabiliana na tatizo la upatikanaji wa maji katika maeneo yetu. Ni imani yangu kuwa kila mmoja wetu atatekeleza wajibu wake ili tuweze kutekeleza ibada zetu kwa wepesi huku nafsi zetu zikiwa zimeridhika. Tumuombe Mwenyezi Mungu atushushie baraka zote za Mwezi huu Mtukufu wa Ramadhani.

Ndugu Wananchi,
Tumebahatika kuwa na kitabu cha Quran na Mwezi Mtukufu wa Ramadhani. Pamoja na kuendesha ibada za Saumu, Sala na utoaji Sadaka katika mwezi huu, tutakuwa tumejipangia vyema ikiwa tutazidisha kusoma na Quran pamoja na Hadith za Mtume Muhammad, S.A.W. katika mwezi huu.

Kuporomoka kwa maadili ni miongoni mwa matatizo yanayoikabili jamii yetu siku hizi. Sote tunaelewa madhara yake, yakiwemo maasi, uhalifu, kutotii sheria na hata kuanguka kwa kiwango cha elimu kwetu na kwa watoto wetu.

Tukirejea kwenye Quran na Hadith za Bwana Mtume S.A.W. tutajisaidia kupata ufumbuzi wa kuondosha madhara haya niliyoyagusia. Kwanza tukumbuke kuwa Quran Tukufu inanufaisha kila pahala na kila zama. Aya na sura za Quran zimejaa hekima (Ishara) ya elimu, sayansi, historia, maadili na kila fani. Kwa mfano, Aya ya 53 ya Surat FUS SWILAT, Juzuu ya 24, inatuambia “Tutawaonesha Ishara zetu katika upeo wa mbali katika nafsi zao wenyewe mpaka inabainika kwamba haya ni kweli. Je haikutosha kwamba Mola wako yeye ni Shahidi wa kila kitu?”

Kuhusu elimu katika mwezi kama huu iliteremshwa sura ya amri ya kusoma, aya ya kwanza ya Qurani, iliyosema:
“Soma kwa jina la Mola wako aliyeumba. Amemuumba binaadam kutoka tone la damu. Soma! Na Mola wako ni karimu kushinda wote. Ambaye, amefundisha kwa kalamu. Kamfundisha mtu aliyekuwa hayajui!

Aya hizi zinatuhimiza wajibu wa elimu, zinatufundisha sayansi ya maumbile na zinatupa maarifa ya manufaa ya elimu na utamaduni, yakiwa ni funguo za maendeleo kwetu katika nyakati zote.

Ndugu Wananchi,
Elimu hii haipatikani bila ya kuitafuta. Tukumbuke kuwa Quran imeeleza katika Surat Ibrahim, Aya ya kwanza kuwa:

“Hiki ni Kitabu tulichokiteremsha kwako ili uwatoe watu kwenye kiza uwapeleke kwenye mwangaza kwa idhini ya Mola wao, uwafikishe kwenye njia ya Mwenye Nguvu na Msifiwa”.

Ndugu Wananchi,
Nawasihi muutumie muda mwingi kuisoma na kupata maarifa ya Quran katika Mwezi huu, mafunzo ambayo yatadumu siku zote. Tukumbuke usemi wa Sayyidna Muhammad, Alayhi Salam kwamba:
“Asiyekuwa na chembe ya Quran moyoni mwake ni kama nyumba iliyobomoka”.
Imani zetu zitajengeka na maadili yetu mema yatarejea tutakapoisoma na kujifunza Quran na kuwa wakweli katika maisha yetu ya uongozi na ya kuongozwa. Uelewa wetu utayageuza maisha yetu katika njia sahihi. Baadhi ya wanazuoni wanasema “Elimu bila ya vitendo ni kama mti usiotoa matunda”. Hivyo tuazimie kuyatumia mafunzo ya Ramadhani katika maisha yetu yote ya kawaida kama ni matunda ya Saumu. Matunda ambayo ni muhimu kwetu.
Ndugu Wananchi,
Serikali yetu imo katika juhudi za kuwaandalia wananchi wake maisha bora, kwa kupitia mageuzi ya katiba na pia kwa kuhesabiwa watu, mambo yaliyomo katika sheria zetu. Quran na Hadithi za Bwana Mtume S.A.W zinatufundisha mshikamano, umoja na utiifu wa sheria. Ni vyema kufahamu na kuzingatia usafi wa nia (IKHLAS) ili tuwe watu wema na wenye kupenda amani na tusiokuwa na hasada au kupenda kutukuzwa.

Ndugu zangu nyote ni mashahidi ni mashahidi kuwa nchi yetu inaendelea kupata mafanikio. Uchumi wetu umeendelea kukua licha ya kuwepo kwa changamoto kadhaa. Wananchi na viongozi tumeshikamana kwa lengo moja la kuleta maendeleo ya haraka kwa nchi yetu. Nakunahini nyote tuendelee kushikamana, tuendelee kutii sheria na kujiepusha na vitendo vyote vya uvunjifu wa amani.

Tujikumbushe Surat Al – Imran, Aya 103 inayosema:
Na shikamaneni kwa kamba ya Mwenyezi Mungu nyote pamoja, wala msifarikiane. Na kumbukeni neema ya Mwenyezi Mungu iliyo juu yenu; vile mlivyokuwa nyinyi kwa nyinyi maadui, naye akaziunganisha nyoyo zenu; kwa neema yake mkawa ndugu”.

Ndugu Wananchi,
Tuutukuze Mwezi huu wa Ramadhani kwa kukumbuka mafundisho hayo ya Quran na tuendeleze shughuli zetu za kimaisha katika hali ya amani, utulivu na mshikamano. Pamoja na hayo, tufanye biashara kwa misingi ya kutodhulumiana katika bei, viwango na vipimo.

Kuhusu hili la biashara, sote tunakubaliana kuwa Mwezi Mtukufu wa Ramadhan ni wa neema kibiashara. Lakini ni vyema kufanya neema hii iwe kwa wauzaji na kwa wanunuzi. Muuzaji anauza bidhaa zake nyingi zaidi, kwa hivyo anapaswa kuhakikisha zina ubora na anachuma faida kwa kiasi ya anachouza. Mnunuzi naye anahitaji kupewa bei iliyo nafuu, hasa kwa bidhaa ambayo Serikali imeipunguza kodi, kwani Serikali yenu kama kawaida itapunguza ushuru kwa bidhaa muhimu za chakula ili kuwawezesha wananchi kupata unafuu wa bei.

Wakati huo huo, ni jambo la kusikitisha kuona baadhi ya wafanyabiashara wenye tamaa wanasafirisha bidhaa kama vile unga, sukari na mchele waliotozwa kodi ya chini na kuzisafirisha kwa njia ya magendo nje ya Zanzibar ili wapate faida kubwa. Kwa hakika jambo hili linasababisha upungufu wa baadhi ya vyakula na kuwasababishia shida wananchi wakati huu wa mwezi wa Ramadhan. Tunapaswa kuwa waadilifu katika hili na pia katika kuhakikisha vipimo vya kuuzia ni vya halali. Serikali imeweka mazingira mazuri ya biashara hasa katika Mwezi huu Mtukufu na ni wajibu wetu kuyatumia vyema ili tunufaike sote. Kama kawaida Serikali itakuwa macho kuona biashara inaendeshwa kwa mujibu wa sheria na kujali maslahi ya wananchi.

Natoa wito tuwe watendaji wema na ihsani baina yetu na hasa kwa masikini na wasiojiweza. Utoaji sadaka ni jambo la msingi na hatuna budi kulizingatia zaidi katika Mwezi huu, ili wenzetu wenye kipato cha chini nao mwezi huu wa Ramadhan uwe ni mwezi wa furaha kwao. Ramadhan Karim – basi tuwe na ukarimu kwa wenzetu na wageni wetu.

Aya 29-30 ya Surat Faatir inasema: “Hakika wale wanaosoma kitabu cha Mwenyezi Mungu na wakashika sala, na wakatoa kwa siri na kwa dhahiri katika tulivyowaruzuku, hao hutaraji biashara isiyobwaga; ili yeye amalize ujira wao kwa ukamilifu, na awazidishie kutokana na fadhila zake. Hakika yeye ni mwenye kusamehe, Mwenye shukurani”.
Nawasihi ndugu zetu wafanya biashara, wakulima, wavuvi na wahusika wote kuzingatia mambo hayo ili sote tuwe tumepata nafuu. Kutokana na hali nzuri ya hewa natumai tutakuwa na mwezi wa neema.

Ndugu Wananchi,
Kwa kuwa Ramadhani mwaka huu imetujia katika msimu wa Watalii na ziara za Wazanzibari wenzetu wanaoishi nchi za nje, tunapaswa kwa umoja wetu kuwaonesha wema wetu na mambo mema kwao. Tudumishe sifa yetu ya ustaarabu, uvumilivu na ustahamilivu, tushikamane nao na tuwaelimishe kwa upole kwa yale wasiyoyajua ya mila zetu. Tudumishe amani na tuhakikishe usalama kwa watu wote, hasa nyakati za usiku ambapo watu wengi wanakwenda misikitini kufanya ibada za Mwezi wa Ramadhan.

Sote kwa pamoja tujitahidi kuweka mitaa yetu katika hali ya usafi na Mamlaka zinazohusika na usafi ziongeze bidii kusafisha maeneo ya makazi na matembezi ya watu.

Tujitahidi kuzingatia mafundisho ya dini katika kupata ukamilifu wa saumu zetu. Wananchi wengine wasiowajibika na saumu kama kawaida watoe ushirikiano na wawe wastahamilivu kwa wenzao wanaofunga. Wale wasiowajibika kufunga kwa sababu mbali mbali wajitahidi kutumia fursa hii vyema bila ya kuwakirihisha wengine. Kwa upande wa madereva na watumiaji wote wa barabara tuzingatie usalama barabarani hasa wakati wa jioni ambapo watu wengi huwa wanakimbilia kuftari.
Jeshi letu la Polisi litaendelea kuimarisha ulinzi wa watu na mali zao kwa kushirikiana na vijana wa ulinzi shirikishi ili wananchi wapate utulivu na watekeleze saumu kwa amani. Ni wajibu tushirikiane na Jeshi letu la Polisi katika kulifanikisha suala hili.
Ndugu Wananchi,
Kwa kumalizia, napenda kugusia mambo mawili. Kwanza ni kwa wazazi na walezi kuzisimamia zaidi nyenendo za watoto wao katika Mwezi huu na kuwahimiza zaidi katika ibada na darsa. Pili, kwa vile tunakabiliwa na msimu wa Hijja, basi ni vyema kwa wanaofanya safari za Hijja kuwa na ushirikiano wa karibu ambao utaleta manufaa kwa wenye kukusudia kutekeleza ibada ya Hajji na Umra. Mwenyezi Mungu awape taufik wote na awafikishe kutimiza azma zao na kuwarejesha nyumbani kwa salama.
Namuomba Mwenyezi Mungu atuwezeshe kutekeleza ibada za Saumu na nyenginezo katika hali ya umoja, mshikamano, amani na utulivu. Atuongezee mapenzi baina yetu ili tuzidi kuhurumiana. Atufanyie wepesi katika kupata riziki za halali na kumshukuru Mola wetu. Tunamuomba Mola wetu atuzidishie imani zetu kwake na tuwe wenye kujali maslahi ya wenzetu na tuwe watu wa kufanya ihsani ili tupate mavuno ya mwezi huu Mtukufu wa Ramadhan.
R A M A D H A N K A R I M
Assalam Aleykum Warahmatullah Wabarakatuh
Ahsanteni sana kwa kunisikiliza.

MAITI ZILIZOPATIKANA KATIKA AJALI YA MV SKIGET ZAANZI KUZIKWA

Baadhi ya Maiti zilizookolewa kutoka katika Meli iliozama na kukosa watu wake zikipelekwa kuzikwa na Serikali katika Eneo la Kama lililotayarishwa makusudi kwa ajili hio.

WANAFUNZI WA SHULE YA MSINGI TANDALE

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mh.Lazaro Nyalandu Atembelea Msitu wa Hifadhi ya Kazimzumbwi Ulioko Wilaya ya Kisarawe Mkoani Pwani

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mh.Lazaro Nyalandu alitembelea Msitu wa Hifadhi ya Kazimzumbwi ulioko wilaya ya Kisarawe mkoani Pwani kujionea uharibifu wa mazingira unaofanywa na kikundi cha watu wanaotaka kujitwalia maeneo ndani ya msitu kuanzisha makazi yao.

akizungumza baada ya kujionea uharibifu huo na kukagua mipaka kama inavyoelekezwa na Tamko la Serikali no 306 la Septemba 1954 ambalo lilianzisha rasmi msitu huo wa hifadhi kwa ajili ya kulinda na kuhifadhi vyanzo vya maji kwa wakazi wa mikoa ya Dar es salaam na Pwani na vizazi vijavyo.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Nyalandu akizungungumza na Waandishi wa habari alioambatana nao.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mh.Lazaro Nyalandu akipitia ramani ya eneo hilo la Msitu wa Kazimzumbwi.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mh.Lazaro Nyalandu akipatiwa maelezo na Mmoja wa viongozi wa Wilaya ya Kisarawe juu ya Msitu wa Kazimzumbwi.

Popular Posts