Pages

Thursday, November 8, 2012

Rais Jakaya Kikwete Azindua Rasmi Ujenzi wa Bomba la Gesi Asilia toka Mtwara hadi Dar es salaam


Rais Jakaya Mrisho Kikwete akizindua rasmi ujenzi wa bomba la gesi asilia toka Mtwara hadi Dar es salaam leo Novemba 8, 2012 maeneno ya Kinyerezi njijini Dar es salaam. Nyuma yake ni Makamu wa Rais Dkt Mohamed Ghalib Bilali.
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Makamu wa Rais Dkt Mohamed Ghalib Bilali na viongozi wengine wakimsikiliza  Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo miundombinu ya  bomba la gesi asilia toka Mtwara hadi Dar es salaam leo Novemba 8, 2012 maeneno ya Kinyerezi njijini Dar es salaam. Nyuma yake ni Makamu wa Rais Dkt Mohamed Ghalib Bilali.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na ujumbe wa kampuni inayojenga bomba la gesi asilia kutoka Mtwata hadi Dar es salaam, Benki ya Exim ya China na viongozi waandamizi wa serikali alipowakaribisha Ikulu kwa mazungumzo baada ya uzinduzi rasmi wa ujenzi wa bomba hilo maeneo ya Kinyerezi jijini Dar es salaam.Picha na IKULU

U.S. Ambassador to Tanzania Alfonso E. Lenhardt resent's ambulance keys to the Chief of Medical Services of the Tanzania Peoples Defense Force (TPDF), Major General AS Mwabulanga


  U.S. Ambassador to Tanzania Alfonso E. Lenhardt (right), present's ambulance keys to the Chief of Medical Services of the Tanzania Peoples Defense Force (TPDF), Major General AS Mwabulanga, (left), during a donation ceremony held yesterday at the TPDF Headquarters in Dar es Salaam.
US Ambassador to Tanzania, Alfonso E. Lenhardt, (fourth from right), Chief of Medical Services of the Tanzania Peoples Defense Force (TPDF), Major General AS Mwabulanga, (fourth from left) following the donation ceremony by the United States yesterday at the TPDF Headquarters in Dar es Salaam. Others officials pictured are Country Director, Walter Reed Army Institute of Research (WRAIR), Edward Sekonde, (right); Master Chief, Operations Coordinator, Defense Attaché Office, Vladimir T. Narvaez, (second from right); Brigadier General LS Msangi, (third from right); and Colonel DB Maganga, (left); Senior Defense Official/Defense Attache, Lieutenant Colonel, Kevin C. Balisky, (second from left); and General Officer Command of General Military Hospital Brigadier General VT Lyimo, (third from left).

UBORESHAJI WA MIUNDOMBINU MKOA WA DODOMA


 Barabara za katikati ya mitaa ya manispaa ya Dodoma zikiwa zinatengenezwa kwa kiwango cha Lami.
Wajasiriamali wakiwa wameweka biashara zao kwenye moja ya mageti ya makao makuu ya CCM,kipindi hiki cha mkutano mkuu kumekuwa na maongezeko ya mahitaji ya bidhaa za chama bora Tanzania,hivyo kutoa fursa kwa wafanya biashara wengi kuuza bidhaa za chama hicho.Picha na Adam Mzee-Dodoma

Nigeria: Don’t Shoot the Messenger When You Should be Addressing Human Rights Abuses


By Amnesty International
Nigeria: Don’t Shoot the Messenger When You Should be Addressing Human Rights Abuses
8 November 2012
The attack by senior Nigerian officials on an Amnesty International report that documents human rights violations by the country’s police and military is a diversionary tactic – shooting the messenger when the security forces should really be concentrating on putting their house in order.

Anyone who reads the report, Nigeria: Trapped in the Cycle of Violence, will see that Amnesty International condemns the unlawful actions of Boko Haram in just as strong terms as it does those of the government forces.
The report fully reflects Amnesty International’s fundamental commitment to objectivity and impartiality in research, analysis and advocacy of human rights issues.
Researchers for Amnesty International interviewed victims of violence perpetrated by both Boko Haram and the security forces in compiling the report. They spoke to judges, magistrates, doctors, teachers, health and education professionals, journalists, lawyers and representatives of non-governmental human rights organizations.
The final report presents research gathered during numerous visits to Nigeria over two years between 2010 and 2012. It includes information gathered via telephone interviews and draws on court cases, legislation, policy documents, medical reports and video and photographic evidence.
It also includes information provided by representatives of the military, the police and several branches of government following meetings with representatives of Amnesty International in July 2012 to discuss the preliminary findings and observations.

In August 2012 a nine page briefing was sent by courier to security and government authorities in Nigeria containing Amnesty International’s findings and a list of over 90 cases, including names, arresting authority and other relevant information.

The briefing included requests for the cases mentioned to be investigated and invited response and comment.  None was received even though Amnesty International would have reflected any comments in the final report.

Full names of victims were not included in the public report published in November to protect the individuals involved.
The Honourable Attorney General of the Federation (HAGF), on behalf of the President of Nigeria and commander-in-chief of the Nigerian Armed Forces, met Amnesty International on 1 November 2012 following the official launch of the report. He stated that all allegations of human rights violations by security forces would be investigated and that Nigeria was committed to ensuring its security forces operate at all times within the rule of law and with respect for human rights.

The HAGF also stated that any state actors found to have violated human rights would be brought to justice. Amnesty International welcomes this statement and hopes that the authorities will take immediate and concrete action to address the real problem and commit to carrying out a full investigation into human rights abuses and violations and to bring perpetrators to justice.

The Nigerian government and the security forces should recognize that the population will not be truly secure until everyone in Nigeria can be confident not only that the risk of attacks from Boko Haram has been reduced, but also that they will not face human rights violations at the hands of the very state security forces mandated with their protection.
Background

Amnesty International’s meetings with army, police, ministers and officials included the Minister of Police Affairs, the Minister of Interior, the Senior Special Assistant to the Honourable Attorney General of the Federation, the Inspector General of Police, representatives from the Office of the National Security Adviser, the Defence Headquarters Spokesperson and the Commissioner of Police for Borno state.

In August 2012 our briefing was sent to – and according to the courier company – received by the following offices:
- Hon. Minister of Police Affairs, (delivered 27 August, 12:34);
- Hon. Attorney General of the Federation, (delivered 27 August, 12:00);
- Hon. Minister of Interior (delivered 27 August, 11:20);
- Hon. Minister of Foreign Affairs; (delivered 27 August, 12:58);
- National Security Adviser (delivered 31 August, 10:30);
- Defence Headquarters, (delivered 27 August, 12:50);
- Inspector General of Police, (delivered 27 August, 14:20);
- Director-General of the State Security Service (SSS) (delivered 29 August, 16:25);
- Comptroller General of Prisons (delivered 28 August, 10:56);
- Commissioner of Police Borno State, (delivered 29 August, 12:00)
- Commissioner of Police Kano State, (delivered 27 August, 11:17).

A briefing was also sent to the Commander of the JTF Borno state but this was returned marked “refused delivery.”

SIFA ISHIRINI ZA KIONGOZI BORA


Usomi wa ngazi mbalimbali si sifa ya mtu kufaa kuwa kiongozi, dunia katika historia yake ina majina lukuki ya baadhi ya viongozi ambao walikuwa wasomi, lakini hatima ya uongozi wao haikutofautiana na wajinga.
Bila kwenda mbali na tuangalie hata hapo nyumbani Zanzibar kuna baadhi ya viongozi serikalini, kwenye mashirika kwenye Baraza la wanaotuwakilisha na hata kwenye sekta binafsi ambao wakikuonesha vyeti vyao vya unaweza kuogopa, lakini utendaji wao ni kichefuchefu.
Kisaikolijia sifa za kiongozi ziko wazi na ni muhimu, mtu kuwa nazo kabla au baada ya kupewa cheo. Leo tunataka kuziangalia kwa undani sifa hizi, ili kama wananchi au viongozi wenye dhamana ya kuchagua watu wa kuongoza tuwatazame watu kwa sifa zao kabla na baada ya kuwapa nafasi. Sifa za kiongozi ni hizi zifuatazo:
Awaze mafanikio makubwa
Kiongozi bora lazima awe na maono ya juu ya kuhakikisha kuwa nchi yake, kampuni yake sekta yake inapata mafanikio makubwa, hii ndiyo itakuwa dira ya kazi yake itakayompa muongozo wa kusimamia wafanyakazi na watendaji wote walio chini yake kufikia kiwango cha mafanikio anachokiwaza. Kiongozi asiyekuwa na mawazo ya juu ya kuendelea kutoka mahali alipo hafai.
Awe na nia
Haitoshi kwa kiongozi kuwa na mawazo chanya peke yake bila kuwa na nia ya kuyatimiza. Hivyo, kiongozi atafaa kuchaguliwa kuwa kiongozi endapo tu atakuwa na uwezo wa kuratibu vyema na kutekeleza alichowaza. Ajue njia anayopita, awatangulie anaowaongoza kwa vitendo.
Ajitambue mwenyewe
Lazima kiongozi ajitambue mwenyewe ni mtu wa namna gani, ajue uwezo wake na upungufu wake na awe tayari kujiongezea maarifa kila siku, ili aweze kukabili changamoto na mabadiliko ya ulimwengu. Asome, afuatilie mambo yanavyokwenda na ajifunze kwa wenzake kuhusu kufanikisha malengo yake.
Asimamie maamuzi
Kuna wakati malengo hukumbana na vikwazo, hivyo ni wajibu wa kiongozi kusimamia maamuzi sahihi na kuwa mtu wa mwisho. Kiongozi mwenye kubadilika badilika kama kinyonga, hafai kwa vile kukosa msimamo kuna maanisha udhaifu wa mipango na kujiamini.
Adhibiti msongo wa mawazo
Tunamtarajia kiongozi mzuri awe ni mtu mwenye kupunguza msongo wa mawazo, ili kuifanya akili yake ifikie maamuzi sahihi, lakini kama atakuwa mwenye kuwaza mengi, atajikuta anachanganyikiwa na kuwa mtu wa jazba katika maamuzi na hivyo kuipotosha jamii.
Akubali kukosolewa
Viongozi wasiokuwa na sifa za uongozi huwa hawakubali kukosolewa, wakidhani kuwa hiyo ndiyo njia ya kuthibitisha msimamo wao na usahihi wao. Kiongozi makini ni yule ambaye atakuwa tayari kukosolewa na kuwapongeza wanaomkosoa kwa kutazama mwenendo wake na usahihi wake. Asiyekubali kukosolewa hafai kuwa kiongozi.
Awe msikilizaji
Kiongozi mzuri ni yule ambaye atakuwa tayari kuwasilikiza watu walio chini yake, apokee maoni yao na ikiwezekana ayafanyie kazi. Lakini pia anatakiwa kuwafahamu kwa undani, ili aweze kuwaongoza vema kufuatana na hali zao. Akiwa na watu walemavu wenye kasoro kadhaa wa kadhaa anatakiwa kuwatambua kabla na baada ya kuwa kiongozi wao. Kuongoza usichokifahamu ni ujinga.
Afuate haki
Kiongozi imara anatakiwa kufuata haki katika kuongoza kwake, asijione mwenye haki zaidi ya wale anaowaongoza katika sheria. Ni muhimu kwake kuwafanya walio chini yake kujiona wako huru katika mawazo na matendo. Kiongozi anayetumia nguvu na ukali kuongoza watu hafai. Hata yule mwenye kujivunia uongozi wake naye hafai.
Awe egemeo la watu
Sifa nyingine ya kiongozi ni kuwa egemeo la watu wake katika shida na raha. Kiongozi mzuri ni yule ambaye atakuwa tayari kusikitika, kuomboleza, kufurahi pamoja na watu wa chini yake bila kujitenga nao. Ajitolee kuwatumikia watu kwa hali na mali na awe tayari kutumika zaidi kwa maslahi ya wengine.
Atie moyo watu
Kiongozi mzuri ni yule ambaye atakuwa na uwezo wa kuwatia moyo walio chini yake ili waweze kuendeleza vipaji vyao. Haipendezi kwa kiongozi kuwavunja moyo watu kwa kauli za kudharau kazi na jitihada zao walizojaribu kufanya katika kutekeleza majukumu yao kama wafanyakazi au wananchi.
Afurahie mafanikio
Sifa nyingine muhimu ya kiongozi ni kuwa tayari kufurahia mafanikio aliyopata pamoja na watu wake. Ni wajibu wa kiongozi kutoa tuzo, kuwashukuru wafanyakazi wake na kuwa tayari kuwapa ofa. Hii itasaidia kuwafanya watu waone hawajapoteza nguvu zao katika utendaji wao na kwamba wanakubalika. Si busara wakati mwingine kuwakosoa watu mbele ya hadhara na kueleza kutofurahishwa na kazi zao.
Aungane na wa chini yake
Mtu kuwa kiongozi haimaanishi amekuwa wa tofauti na watu wengine kiasi cha kushindwa kuchangamana nao kama wanavyofanya baadhi ya viongozi. Kiongozi mwema ni yule atakayeungana na watu wake katika maisha ya kawaida. Kuwa kiongozi haimaanishi kwamba watu watakufuata wewe kila siku, wakati mwingine wewe unatakiwa kuwafuata wao na kuwa nyuma yao hata mahali walipokosea au wanapokabiliwa na makosa, watetee na uoneshe kuwajali na kuwapigania, makosa utayahesabu baada ya utetezi wako kukamilika.
Akubali lawama
Kama kiongozi amefanya mambo ambayo jamii haikupendezwa nayo anachotakiwa kufanya ni kukubali kulaumiwa. Ikiwa anaongoza kitego cha umeme kwa mfano na watu hawakupata nishati hiyo kwa wakati hatakiwi kukwepa lawama, vivyo hivyo kwenye wizara na idara au nchi kwa ujumla.
Afahamu kutatua matatizo
Kiongozi mzuri ni yule ambaye atakuwa na uwezo wa kuzuia migogoro na kuitatua kwa haraka. Muongozo mzuri katika eneo hili umesimama katika mawasiliano na watu wa chini, mawasiliano haya ndiyo yatakayomuwezesha kiongozi kujua matatizo waliyonayo wafanyakazi wake au hata jamii anayoiongoza na hivyo kumfanya apate wasaa wa kuyashughulikia mapema.
Ajifunze kwa makosa
Wakati mwingine mawazo na mipango inaweza ikaenda kombo, hivyo ni wajibu wa kiongozi kujifunza kutokana na makosa yake au ya wale anaowaongoza, ili kuepuka kurudia makosa yale yale na kumfanya apoteze sifa za kuwa kiongozi mzuri.
Mwanafalsafa Winston Churchill aliwahi kusema “The price of greatness is responsibility.” Thamani ya ukuu ni uwajibikaji.
Awe mwaminifu
Miongoni mwa maeneo magumu kabisa yaliyowashinda na yanayoendelea kuwashinda viongozi wengi ni uaminifu. Kiongozi bora ni yule ambaye yuko tayari kusimamia muongozo wa katiba ya nchi au marufuku alizowekewa katika madaraka yake. Hii inakwenda sambamba na kutowaonea, kuwanyanyasa wa nchini yake kwa kutumia cheo chake.
Awe mkweli
Viongozi wengi hasa wa kisiasa siku hizi ni waongo hakuna mfano, wamejaa ahadi zisizotekelezeka na hata wanapogundua kuwa hawana uwezo au wamekwama kuzitimiza, hawaoni haja ya kutubu mbele ya wanaowaongoza. Kiongozi makini ni yule atayekuwa tayari kuonesha ubora wa matendo na kauli zake.
Asiwe mwenye majungu
Kuna baadhi ya viongozi kwenye maofisi wanaendekeza sana majungu na pengine kuyapa umuhimu wa hali ya juu. Hii ni sifa mbaya kwa kiongozi yo yote, hivyo anayetumikia ‘umbea’ katika ofisi aliyokabidhiwa kama mkuu anapaswa kuondolewa. Kiongozi makini atatumia uwezo wake kuzuia watu wasimsengenye/wasisengenyane kwa kuwa muwazi na mwenye kufungua milango ya watu kumuona na kumlaumu na kueleza hisia zao.
Awe bora
Kwa kila analofanya kama kiongozi lazima alifanye kwa ubora, asiwe mtu mwenye kulipua kazi na kufanya chini ya kiwango cha uwezo wake. Kila siku katika kazi, maamuzi, usimamizi, utekelezaji lazima atumike zaidi ya uwezo wake.

Waziri Mwakyembe aivunja Bodi ya Bandani na kuunda mpya

Mheshimiwa Dkt. Harrison G. Mwakyembe (Mb.), Waziri wa Uchukuzi, amefuta uteuzi wa Wajube wote wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari (TPA) kuanzia juzi tarehe 06 Novemba, 2012 na kuteua Wajumbe wengine wanane (8) wanaounda Bodi hiyo. Waziri amechukua uamuzi huo kwa mujibu wa mamlaka aliyonayo chini ya Kifungu cha 6(2) cha Sheria ya Bandari na Kifungu cha 1(2)(i) cha Jendwali la Kwanza la Sheria ya Bandari ya 2004.

Waliofutiwa ujumbe wa Bodi ni:

1.       Bwana Dunstan G. Mrutu

2.       Eng. George H. Alliy

3.       Mhe. Alh. Mtutura A. Mturur (Mb.)

4.       Bwana Emmanuel Mallya

5.       Bibi Mwantumu J. Malale

6.       Bibi Maria N. Kejo

Kwa bahati mbaya wajumbe wawili wa Bodi hii walipoteza uhai hivi karibuni. Mungu azilaze roho za marehemu hawa mahali pema peponi, Amina.

Walioteulwa kuingia kwenye Bodi hiyo ni:

1.       Dkt. Jabiri Kuwe Bakari

2.       Bwa. John Ulanga

3.       Bi. Caroline Temu

4.       Bwa. Jaffer Machano

5.       Dkt. Hildebrand Shayo

6.       Bw. Saidi Salum Sauko

7.       Eng. Julius Mamiro

8.       Bi. Asha Nassoro

Mabadiliko haya ni sehemu tu ya hatua ambazo Wizara inachukua kurejesha ufanisi katika Mamlaka hiyo ili iweze kuchangia zaidi kwenye pato la Taifa.

Waziri ameiagiza Menejiment ya TPA kuwapa nyaraka zote muhimu Wajumbe wapya wa Bodi ili wajiandae kabla hajakutana nao ndani ya siku kumi kuanzia juzi ili kuingia nao Mkataba wa Ufanisi (Performance Contract).

Ofisi ya Mawasiliano Serikalini
Wizara ya Uchukuzi
08/11/2012

Source: http://www.wavuti.com/#ixzz2BdXo2XOC

Hoja ya Mhe Halima Mdee aliyoiwasilisha Bungeni ya kusitisha ugawaji wa ardhi

[Chini ya Kanuni ya 54(1) na (2)]

Mheshimiwa Spika,

Kwa mujibu wa Kanuni  namba  54(1) , (2)  na (3) ya  Kanuni za Kudumu za Bunge, Toleo la 2007 naomba kutoa hoja binafsi ya kuitaka serikali  kusitisha zoezi  la ugawaji wa ardhi  kwa wawekezaji ( wa ndani na wa nje)  mpaka hapo tathmini  ya kina itakapofanyika  kuweza kubaini ni kiwango gani cha ardhi kiko mikononi  mwa wawekezaji.

Mheshimiwa Spika,

Katika miaka ya hivi karibuni, kufuatia mtikisiko wa uchumi duniani uliokwenda sambamba na upungufu wa chakula , tumeshuhudia wimbi kubwa la  wawekezaji kutoka nje ,wakinunua au kumilikishwa maeneo makubwa ya ardhi nchini, kwa maelezo kwamba wana nia ya kuwekeza kwa manufaa ya wananchi wenyeji  na Taifa  kwa ujumla , hali ambayo itaweza saidia upatikanaji wa ajira , kukuza uchumi na  kupunguza umasikini . 

Kwa kadiri gharama za Chakula na uhitaji wa Chakula duniani unavyoongezeka ndivyo na kasi ya mahitaji ya ardhi yanavyoongezeka , wawekezaji  wanaona ardhi kama biashara nzuri na yenye tija katika miaka ya baadae. Na kwa nchi tajiri zinazoagiza vyakula toka nje ( China,Japan,Korea ya Kusini ,Saudi Arabia nk.) wanaona umiliki wa mashamba makubwa kama njia ya kujihakikishia usalama wa chakula katika nchi zao. Na wakati huo huo Makampuni binafsi makubwa ya kimataifa wanaiona hii kama fursa ya kujitanua kibiashara na kutengeneza faida kubwa.

Mheshimiwa Spika,

Inakadiriwa kwamba kati ya mwaka 2001 hadi 2010 kulikuwa na maombi ya ardhi zaidi ya hekta  milioni 203 katika nchi zinazoendelea. Hii ni sawa na  maombi ya hekta 55,616 kila siku katika kipindi cha miaka 101 Halikadhalika nchini Tanzania katika miaka ya karibuni takriban  hekta milioni nne zimeripotiwa ‘kuombwa’ na  wawekezaji wa nje  kwa kilimo cha mazao  ya mafuta (AGROFUEL) na Chakula.  

Mheshimiwa Spika,

Kasi ya maombi ya ardhi ,na hatimaye kumilikishwa ardhi   wageni, imegeuka shuruba kwa wananchi , wengi wao wakiwa ni wakulima wadogo wadogo ambao wamejikuta wakiondolewa  kwa katika  maeneo yao ya asili  ili kuwapisha  wageni. Wengi wao wakiachwa hohe hahe, na katika lindi la umasikini mkubwa. Hii inatokana na ukweli kwamba kumekuwa na tafsiri ambayo sio sahihi, kwamba ardhi wanayopewa wawekezaji haina wenyewe/haina mtu /haitumiki . Wakati ukweli ni kwamba maeneo mengi kama sio yote yalikuwa yanatumiwa n a wakulima wadogo .

Mheshimiwa Spika,

Hali halisi inaonyesha kwamba , ni sehemu ndogo sana ya ardhi inayochukuliwa  na wageni inatumika kwa manufaa ya kutatua/kupunguza matatizo ya njaa katika nchi husika . Hali kadhalika maeneo mengi ardhi yanayochukuliwa na wawekezaji hao  huwa hayaendelezwi kama inavyopasa , na yale ambayo yanaendelezwa , yanaendelezwa kwa kiwango kidogo sana huku wananchi wengi wakiachwa pasi na ardhi ya kutosha kwa kilimo. Na katika hatua nyingine, wawekezaji baada ya kupata /kumilikishwa ardhi kwa bei ya kutupa, hawaitumii,wanasubiri ipande thamani  , kisha kuiuza kwa faida kwa wawekezaji wengine.

Mheshimiwa Spika,

Ninaliomba  Bunge lako tukufu , likubaliane na hoja ya kuitaka  Serikali kusitisha zoezi la ugawaji wa ardhi ili kuweza kutoa fursa ,kama nchi kuweza kujitahmini kwa kina, wapi tulikosea ili tuweze kujipanga upya kwa manufaa ya nchi na wananchi. Hii inatokana na ukweli kwamba hata wizara ya ardhi leo wakitakiwa kutoa taarifa sahihi ya ardhi kiasi gani iko chini ya miliki ya wageni,hawana takwimu sahihi,zaidi ya zile chache zilizopatikana kupitia Tanzania Investment Centre (TIC) na ambazo pia zimethibitika kuwa na mgogoro mkubwa kutokana na taratibu kutofuatwa.

Mheshimiwa Spika,

Mifano mingi inaonyesha kwamba  kumekuwa na ubabaishaji mkubwa sana na kuumizwa sana kwa wananchi , na  mbaya zaidi katika mazingira mengine serikali imekuwa kuwadi wa wawekezaji dhidi ya wananchi wake. Kuna haja kubwa kwa waheshimiwa wabunge kutambua kuwa matatizo ya ardhi yanayoikumba Rufiji, Kilombero, Bagamoyo, Kisarawe na lugufu yanaikumba pia Muheza, Pangani, Katavi ,Meatu, Kinondoni, Njombe na Ngorogoro. Hivyo basi kuna haja kubwa ya kujenga mshikamano  kwa kuunganisha nguvu ili kulinda maslahi na rasilimali za umma. Nitatoa mifano michache, kuonyesha uzito wa tatizo hili:

Bonde la Mto Rufiji (Rufiji River Basin)

Hili ni eneo lenye ukubwa wa Km za mraba 176,000. Linajumuisha Rufiji Delta, Luwero,Kilombero na Mto Ruaha..93% ya wakazi wa maeneo wanaozunguka  eneo hili wapatao 500,000 wanajishughulisha na kilimo, kama wakulima wadogo wadogo. Kutokana na umuhimu na unyeti   wa eneo husika kumekuwa na wimbi kubwa la makampuni ya kigeni, wakipeleka maombi moja kwa moja kwenye vijiji au kwa kupitia baadhi ya vyombo vya serikali (RUBADA- Rufiji Basin Development Authority) ambavyo vimeacha majukumu yake na kugeuka kuwadi wa wawekezaji. 

Mheshimiwa Spika,

Makampuni yafuatayo; ( SEKAB  Tanzania Ltd (Sweden), African Green OIL Ltd , SAP Agriculture Ltd (Turkey ), RUBADA na Korean Rural  Community Corporation , Kilombero Plantation  Ltd ( British) , Kilombero Valley Teak  Co. Ltd ( British) , Kilombero Sugar Co. Ltd  (South Africa) , Kilimo cha Yesu ( Uswiss), na Eurovistas (India)  ni kati ya makampuni yaliyomilikishwa ardhi iliyokuwa  inatumiwa na wanakijiji kwa shughuli za kilimo. Wengi wao wakitolewa kwa nguvu ili kuwapisha wawekezaji kwa kurubuniwa kwa kauli tamu.Wakiahidiwa kuletewa maendeleo. Ahadi ambazo nyingi zimegeuka za uongo huku tayari vijiji vikiwa vimepoteza uhalali wa kutumia ardhi yao.

Mheshimiwa Spika,

Taarifa zinaonyesha kwamba katika ukanda huu , ukiacha makampuni ya  Kilimo cha Yesu (Uswis) na Kilombero Sugar Co, kilombero Plantation Co na Kilombero Valley Teak(British), wawekezaji wengine waliokabidhiwa maelfu ya ardhi ya watanzania wameyaendeleza kidogo sana au kuyatelekeza kabisa mashamba ! inawezekana wakisubiri ardhi ipande thamani wawakabidhi wenzao kwa gharama kubwa .2 

Kisarawe:

Sun Biofuels Ltd ni kampuni ya kiingereza inayojishughuliza na kilimo Jatropha . Wanahisa wake wakubwa  ni kampuni ya Sun Biofuels Plc ya Uingereza yenye hisa 88% , Julian ozanne ( mwingereza) mwenye hisa 10% na watanzania wawili, Daudi Makobore  na Herbert Marwa wenye hisa 2% (yaani 1% ).

Inasemekana mwekezaji huyu  alipanga kuwekeza  kiasi shilingi bilioni 25.3 za kitanzania, lengo likiwa kujenga mtambo wa kufulia mafuta  na kilimo cha Jatrofa ( pamoja na mihongo kwa ajili ya kuwalisha vibarua). Ilikadiriwa kutokana na uwekezaji huo zingepatikana ajira za kudumu 1,500 , na ajira za ziada kwa vibarua hasa wakati wa uvunaji.

Mwaka 2009 Kampuni ilifanikiwa  kupata eneo lenye ukubwa wa hekta 8,211 kutoka vijiji 11 vya ( Mtamba, Muhanga, Marumbo,Palaka, Kidugalo, Kurui (40% ya eneo la kijiji lilichukuliwa ),Mtakayo, Vilabwa , Mitengwe, Mzenga ‘A’ and Chakaye. Hata hivyo mwezi  Oktoba 2011, mradi husika ulisamama kutokana na ukosefu wa fedha, na mustakabali wa ardhi ya  kijiji haujulikani.

Mwanakijiji mmoja wa kijiji cha  Palaka , Kisarawe alinukuliwa akisema  kwamba walikubali kuwaachia ardhi wawekezaji kwa mdomo, pasi kuandikiana popote kwa sababu waliaziamini ahadi zao za kutoa huduma za jamii i.e maji, barabara,shule nk, lakini hakujua kiasi gani cha eneo lake kinapaswa kuchukuliwa kwa sababu hawakuwa na nyaraka zozote za kuonyesha mipaka ya shamba lake. Hakuwa anafahamu haki zake za kisheria,hivyo hakujua madhara ya kile alichokikubali mpaka alipopoteza ardhi yake yote bila  kulipwa fidia.3 

Mwananchi mwingine wa kijiji cha Kurui, alinukuliwa akisema kuna tofauti kubwa kati ya makubaliano ya kutoa ardhi na kushiriki  katika mkutano wa kijiji. Anadai kwamba kushiriki kwao katika kikao cha kijiji ,kulichukuliwa kama kukubali kutoa maeneo yao . Hakuingia makubaliano na mtu yeyote kutoa eneo lake.4 Eneo lilichukuliwa na mwekezaji , majina ya mahudhurio yalitumika kama kielelezo kuonyesha kama waliafiki,wakati hawakufanya hivyo.

Rukwa:

Mheshimiwa Spika

Eneo hili ,linahusisha Hekta 80,317 (Katumba) na 219,800 ( Mishamo) kwa ajili  ya Kampuni ya kimarekani ya Agrisol . Majadiliano yanaratibiwa na viongozi wakubwa  sana Serikalini. Mradi huu umejikita kwenye uendelezaji wa mashamba makubwa , na matumizi ya mbegu zenye viini tete (GMO). Ili kufanikiwa kwa mradhi huu wakulima wadogo wadogo wapatao 162,000 walitakiwa kuhama kumpisha mwekezaji huyo wa kigeni. 

Licha ya kelele nyingi kupigwa juu ya makosa ya kiufundi ambayo serikali inayafanya kwa kutaka kulikabidhi eneo kubwa na lenye rutuba kwa wageni , na licha aliyekuwa mshirika muhimu wa Agrisol IOWA State University College of Agriculture ,aliyekuwa mhimili muhimu wa mwekezaji huyu hasa katika kuwasaidia wakulima wadogo kujitoa baada ya kugundua kwamba mwekezaji huyu hana dhamira ya kuisaidia nchi na wakulima wadogo zaidi ya kujinufaisha kibiashara. Na kwamba alikitumia Chuo husika ili apate uhalali wa kukubalika kirahisi kama mwekezaji mahiri. Serikali inaonekana bado imeziba masikio! 

Kigoma

Wawekezaji walionunua ardhi mkoa wa Kigoma ni Agrisol na FELISA.

FELISA amenunua ekari 3000 katika wilaya ya uvinza kijiji cha basanza kata ya uvinza. Wawekezaji hawa wamewakuta wakulima na wafugaji katika maeneo haya. Wafugaji na wakulima wakagoma kuondoka kwakuwa walikuwa wakiendesha maisha Yao kutegemea ardhi hiyo Huu ni ushahidi dhahili kuwa hakuna ziada ya ardhi ukilinganisha na mahitaji. Mwekezaji kwa kushirikiana na vyombo vya dola alianza zoezi la kuwatoa wananchi mwezi Mei mwaka huu akitumia vikosi vya mgambo kupiga wananchi, kuchoma nyumba, kuharibu mazao na halikadhalika kuwafungulia wananchi mashtaka!

USHAHIDI ZAIDI KUHUSU MGOGORO HUU TAYARI KUNA KESI MAHAKAMA YA MWANZO MWANDIGA KIGOMA KATI YA WAKAZI WANAOGOMA KUHAMA NA MWEKEZAJI. 

 
AGRISOL

Mwekezaji huyu amepewa hekta elfu 10,000 eneo la Lugufu. Eneo hili ndio ili kuwa kambi ya wakimbizi. Na eneo hili ndio limetengwa kuwa Makao makuu ya wilaya . Kwa mujibu wa Mbunge wa Kigoma Kusini (ambaye eneo lenye mgogoro liko ndani ya jimbo analoliwakilisha), Mhe David Kafulila alipozungumza  na watendaji wa halmashauri walikiri kuwepo shinikizo kutoka ngazi za juu.

Na hii inatokana na mantiki ya kawaida tu kuwa uamuzi wa kumpa mwekezaji huyu Eneo hili ni Sawa na kuamua Makao makuu ya wilaya ya uvinza yazungukwe na shamba na mwekezaji. Hivyo mji ambao ni Makao makuu hautatanuka kwasababu utakuwa eneo dogo sana lililozungukwa na shamba. Nasema eneo dogo kwasababu mpaka sasa haijafahamika Makao hayo makuu yatawekwa wapi wakati eneo lote kashapewa mwekezaji. Labda serikali imwombe Agrissol eneo la kujenga wilaya. 

Mheshimiwa Spika,

Zaidi ya mkanganyiko huo pia kuna tatizo la mahitaji ya ardhi, wakazi wa eneo la jirani,wanaotoka Uvinza na Mwamila wanahitaji kulima katika eneo hili lakini wanazuiwa. Taarifa ya mahitaji ya eneo hili kwa wakulima wakawaida ipo ofisi ya mkuu wa mkoa Kigoma.Mkuu wa Mkuu wa Mkoa anakiri kuwa ni tatizo, na kupendekeza labda watu walime kwa muda wakati mwekezaji hajafika. Wakazi mwamila walifanya jaribio la kutaka kulima mwaka huu wakafukuzwa. 

Mheshimiwa Spika,

Mchakato mzima wa agrossol kupewa eneo halikuridhiwa na  wana kijiji,halmashauri na wataalamu walishinikizwa. Na isisitizwe kuwa uamuzi huu unakinzana na juhudi za serikali yenyewe kusukuma wananchi katika kilimo kwani wilaya ya uvinza Hivi sasa mbunge amekopa trekta nne ili kusukuma kilimo kwa yeye kulima na wananchi kulimiwa kwa bei ya chini kuliko bei ya serikali.Halmashauri awali ili kuwa na kituo chenye trekta mbili hapo lugufu Kama kituo cha huduma ya matrekta ya kilimo kwanza, pia halmashauri imenunua trekta tano kwa ajili ya kusukuma kilimo wilaya hii. Juhudi zote hizi ambazo ni matunda ya mkopo ya SUMA JKT, INAKWAMISHWA NA UAMUZI WA SERIKALI KUUZA ARDHI.

Mheshimiwa Spika,

Ni muhimu ikaeleweka kwamba,hakuna anayepinga umuhimu wa uwekezaji, lakini ni muhimu vile vile ikaeleweka kwamba hatutaweza kuendelea kama tukikabidhi kila kitu kwa wageni. Sote tunajua ni kwa namna gani dhahabu, almasi  na Tanzanite zimetumika kujenga uchumi wa mabeberu! Hatuwezi kufanya makosa tena kwenye rasilimali hii muhimu ya ardhi  inayopanda thamani kwa kasi sana! Uchumi hauwezi kuachwa uendeshwe na watu wa nje!

Mheshimiwa Spika,

Kutokana na uwekezaji kutoka nje wa makampuni makubwa uchumi wa Tanzania unarekodiwa kukua kwa asilimia 7. Hiki ni kiasi kikubwa kinachoifanya nchi hii kuwa miongoni mwa nchi 20 kileleni kwa kasi kubwa ya ukuaji wa uchumi dunia lakInI wakatihuohuo inasikitisha kuona nchi hii ni miongoni mwa nchi 20 duniani. Hii inatokana na ukweli kuwa kilimo kinachoajiri 70% ya watanzania kimeachwa, njia ya kuondoka kwenye mlinganyo(equation) hiyo ni ARDHI. wakulima wadogo wagawiwe ardhi, wawezeshwe zana na ufundi kwa kilimo. 

Mheshimiwa Spika,

Mambo kadhaa yamejitokeza :


  1. Uvunjwaji wa haki za binadamu
  2. Kutokuzingatiwa kwa sheria inayotaka wananchi ,waarifiwe mapema washirikishwe na kupewa taarifa sahihi , ili wafanye uamuzi ulio sahihi kwa maendeleo yao (the principle of free ,prior and informed concent-FPIC)-kuhusiana na mradi husika.
  3. Mikataba iliyotawaliwa na usiri mkubwa, na wakati mwingine sheria za nchi kupuuzwa .
  4. Serikali kulipwa fedha kidogo sana. Wastani wa gharama ya kukodi ardhi ni shilingi 200 kwa hekta kwa mwaka. Na muda wa kukodisha ardhi kisheria ni miaka 99.Gharama hii haijalishi eneo shamba lilipo au mazao yanayozalishwa.
Mheshimiwa Spika,

Inawezekana kabisa Tanzania tukawa hatujafikia  hali mbaya kama ilivyo kwa nchi nyingine.....zaidi ya 30%  ya ardhi ya Liberia imekabidhiwa kwa wakulima wakubwa  wa Nchi za magharibi katika kipindi cha miaka mitano! Halikadhalika katika nchi ya Cambodia , inakadiriwa  linalokadiriwa kuwa 56-63% ya ardhi yote inayotumika kwa Kilimo iko mikononi mwa makampuni binafsi ya kigeni. Hivyo basi Serikali ya Tanzania ina fursa ya kujipanga mapema,kabla hali haijawa mbaya! Lazima kuwe na mjadala mpana wa kitaifa ili tuweze kupata njia bora ya kusonga mbele.Hatuta kuwa wa kwanza kufanya hivyo. Jirani zetu wa Msumbiji  wa Msumbiji wamefanya hivyo, halikadhalika serikali ya Papua New Guinea ! 

Ni muhimu kufanya maamuzi sasa . Maamuzi tutakayoyafanya sasa yatakuwa na athari chanya ama hasi kwa kizazi kijacho . Inakadiriwa ifikapo mwaka 2050 watanzania tutakuwa milioni 150, kama leo ardhi yetu tunagawa kwa wageni kwa muda wa miaka 99, tunaweka akiba gani kwa kizazi kijacho? Nini usalama wa Chakula na Uchumi kwa Tanzania ya kesho?

HOJA BINAFSI KUHUSU KUSITISHA UGAWAJI WA ARDHI KWA WAWEKEZAJI HADI TATHMINI YA KIASI CHA ARDHI ILIYOGAWANYWA UTAKAPOFANYIKA

[Chini ya Kanuni ya 54(3)]

Mheshimiwa Spika,

Kwa kuwa rasilimali ardhi ndio urithi pekee wa asili wa mtanzania katika kujitafutia riziki na kuendesha maisha yake;

Na kwa kuwa  idadi ya watu inaongezeka wakati ukubwa wa ardhi hauongezeki jambo ambalo linaonesha dhahiri kwamba kuna hatari ya kiasi cha ardhi kilichopo kisitosheleze mahitaji halisi ya wananchi;

Na kwa kuwa kumekuwa na ugawaji ardhi kwa wawekezaji hasa wa nje  usiojali mahitaji ya ardhi kwa wananchi siku za mbeleni;

Na kwa kuwa  imebainika kwamba  uwekezaji  katika ardhi unaofanywa na makampuni ya nje haujawasaidia wananchi kwa maana ya fursa za ajira na upatikanaji wa chakula kwa kiwango kilichoahidiwa na Serikali na makampuni hayo;

Na kwa kuwa ugwawaji huu wa ardhi kwa wawekezaji unakwenda sambamba na ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu ikiwa ni pamoja na wananchi waliokuwa katika maeneo hayo kupigwa, kuvunjiwa nyumba zao na kufukuzwa bila kulipwa fidia;

Na kwa kuwa kwa kiasi kikubwa zoezi la ugawaji ardhi kwa wawekezaji linakiuka sheria za nchi ambazo zinataka wananchi waarifiwe mapema juu ya ugawaji huo wa ardhi na kushirikishwa kikamilifu ili waweze kufanya maamuzi sahihi kwa maendeleo yao jambo ambalo halifanyiki;

Na kwa kuwa mikataba ya ugawaji wa ardhi inafanyika kwa usiri mkubwa  jambo ambalo linaashria mazingira ya rushwa na kutia shaka kama maslahi ya nchi yanazingatiwa;

Na kwa kuwa  Serikali inapata kodi kidogo sana kutokana na uwekezaji katika ardhi ( yaani shilingi 200 kwa hekta kwa mwaka) na ikizingatiwa muda wa kukodisha ardhi kisheria ni miaka 99; 

Na kwa kuwa asilimia 80 ya watanzania wanategemea ajira katika sekta ya  kilimo ambacho msingi wake ni ardhi;

Na kwa kuwa Ibara ya 63(2)(c) na (d) ya Katiba ya Jamjhuri ya Muungano wa Tanzania ya 1977 inasema kwamba: “Kwa madhumuni ya utekelezaji wa madaraka yake Bunge laweza; kujadili na kuidhinisha mpango wowote wa muda mrefu na wa muda mfupi unaokusudiwa kutekelezwa katika Jamhuri ya Muungano, na kutunga sheria ya kusimamia utekelezaji wa mpango huo; kutunga sheria pale ambapo utekelezaji unahitaji kuwapo sheria”;

HIVYO BASI, naliomba Bunge liazimie:

  1. KWAMBA, zoezi la ugawaji ardhi kwa wawekezaji wa nje na ndani lisitishwe hadi hapo tathmini ya kina itakapofanyika kubaini ni kiasi gani cha ardhi kipo mikononi mwa wawekezaji na wasio wawekezaji.
  2. KWAMBA, tathmini ya kina ifanyike kuweza kubaini raia wa kigeni na wa ndani waliojipatia ardhi kinyemela kupitia serikali za vijiji kinyume na matakwa ya sheria ya ardhi Na. 5 ya mwaka 1999.
Mheshimiwa Spika,

Baada ya kusema hayo, 

Naomba kutoa hoja.

…………………………………..

Halima James Mdee(Mb)

Jimbo la Uchaguzi-Kawe

05.11.2012

1  ILC ( 2011)  ‘Land Rights and the Rush for Land’, http://www.landcoalition.org/cpl/CPL- Synthesis-report.  

2 Land Grabbing in a post investment period and popular  reaction in the Rufiji River Basin. A Research Report by Haki Ardhi,2011. Study carried out  by Dr . Abunuwasi Mwami of the Department of Sociology , University of Dar es salaam and Dr Ng’wanza Kamata of the Department of Political Science , University of Dar es salaam

3 Participant in Community focus Group discussion , Palaka Village , Kisarawe  District , December 3 , 2010 cited in Frederic Mousseau et al . “Understanding  Land Investment Deals in Africa – Country Report Tanzania” 

4 ibid

Source: http://www.wavuti.com/#ixzz2BdUvSF46

Popular Posts